DIDIER Gomes, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa kikubwa ambacho kinawapa nguvu ya kuamini kwamba watapata matokeo mbele ya AS Vita ni pamoja na hali ya kujiamini na maandalizi mazuri. Kikosi cha Simba kinatarajiwa kumenyana na AS Vita kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kuchezwa Aprili 3, Uwanja wa Mkapa. Mfaransa huyo ameongeza kwamba kuchukulia siriazi na kujiamini katika mechi zao ndiyo kitu ambacho kimekuwa kikiwabeba na kuifanya timu hiyo kutopoteza mechi yoyote hadi sasa katika Ligi ya Mabingwa Afrika. Simba ni vinara wa Kundi A la Ligi ya Mabingwa Afrika watakuwa uwanjani kupambana na Vita katika mechi ambayo Simba wakitoa sare tu watajihakikishia nafasi ya kwenda hatua ya robo fainali, lakini Vita wanahitaji ushindi tu ili wafufue matumaini yao ya kutinga robo fainali. Gomes amesema kwamba kila mechi ambayo wamekuwa wakiicheza katika hatua hiyo wamekuwa wakiamini kwamba wanaweza kupata matokeo na hiyo imekuwa msaada mkubwa...
JUMUIYA ya soka kimataifa ‘FIFA’ limetuma salamu za rambirambi kwa shirikisho la soka nchini TFF kufuatia kifo cha Rais, Hayati, Dk.John Pombe Magufuli kilichoripotiwa kutokea siku ya Jumanne, 17 Machi 2021 kwenye Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam kutokana na maradhi ya moyo. Kwa niaba ya wajumbe wa jumuiya ya soka kimataifa, Rais wa jumuiya hiyo Gianni Infatino ameandika kuwa:- “Ilikuwa hisia ya huzuni kupata taarifa za kifo cha Rais Dk.John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. “Tunapenda kuungana na wote wanaotoa salam za pole kutoka pande zote Duniani. Akiongoza toka mwaka 2015, kiongozi mwenye haiba ya juu, aliyetambulika kwa maono yake, uzalendo, matendo ya Utawala bora na kupiga vita rushwa na umasikini, Rais, Dk.John Pombe Magufuli hatosahaulika. “Kwa niaba ya wajumbe wa jumuiya ya soka kimataifa, tunapenda kutoa pole kwa shrikisho la soka nchini Tanzania ‘TFF’, Serikali na watanzania kwenye kipindi hiki kigumu”....
WINGA wa klabu ya Wydad Casablanca ya nchini Morroco, Saimon Msuva amesema kuwa anatamani kukutana na klabu ya Simba katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwani anaamini itakuwa mechi nzuri sana katika msimu huu wa ligi hiyo. Saimon Msuva katika msimu huu wa ligi hiyo akiwa na klabu ya Wydad Casablanca ya Morroco amefanikiwa kuifungia timu hiyo mabao miwili katika michezo minne aliyocheza mpaka sasa. Akizungumzia michuano hiyo Msuva amesema: “Natamani kuona tunakutana na Simba katika hatua ya robo fainali kwani utakuwa mchezo mzuri sana katika ligi ya mabingwa msimu huu kwani itazikutanisha timu bora ambazo zote zinafanya vizuri kwa sasa.
Comments
Post a Comment