UKANDA wa Afrika Mashariki mambo yamekuwa magumu kwenye mechi za kuwania kukata tiketi ya kufuzu kushiriki Michuano ya Mataifa ya Afrika, (Afcon) kwa timu nyingi kuangukia pua. Sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90 dhidi ya Cameroon inaifanya timu ya Taifa ya Rwanda nayo pia kuishia hatua ya makundi. Ni Cameroon na Cape Verde wamekata tiketi ya kushiriki Afcon nchini Cameroon baada ya kuwa nafasi mbili za juu ambapo mwenyeji Cameroon ana pointi 11 huku Cape Verde akiwa na pointi 10. Rwanda ipo nafasi ya 3 na pointi zao ni 6 huku nafasi ya nne ikiwa mikononi mwa Msumbiji wenye pointi 4 baada ya kucheza jumla ya mechi 6. Tanzania pia imeishia hatua ya makundi na pointi zake ni 7 katika kundi J ipo nafasi ya tatu ambapo ni Tunisia wenye pointi 16 na Equatorial Guinea wenye pointi 9 wamepenya mpaka Cameroon. Burundi katika kundi E wapo nafasi ya tatu na pointi zao ni 5 huku Morocco yenye pointi 14 na Mauritania wenye pointi 9 wakitusua mpaka Cameroon. Kenya katika kun...
“WAMEFUNIKA” ndivyo unavyoweza kusema, kwani unaambiwa mastaa sita tu wa kikosi cha Simba wamefanikiwa kufunga mabao 36, ambayo ni idadi sawa na mabao yote yaliyofungwa na nyota wa kikosi cha klabu ya Yanga. Mastaa hao sita wa Simba ni Meddie Kagere, John Bocco, Clatous Chama, Bernard Morrison, Chris Mugalu na Luis Miquissone. Katika mchanganuo huo Kagere amefunga mabao 9 sawa na John Bocco, Clatous Chama 6, Chris Mugalu 5, Miquissone 4 na Morrison 3. Simba ndiyo timu ambayo imefunga mabao mengi zaidi kwenye Ligi Kuu Bara ikiwa na mabao 46 huku yanga wao wakiwa katika nafasi ya pili na mabao 36. Simba pia ndiyo timu iliyofungwa mabao machache zaidi kwenye ligi, mabao 9 ikifuatiwa na Yanga waliofungwa mabao 14.
KOCHA Mkuu wa timu ya Kagera Sugar, Francis Baraza amesema kuwa kazi ya kwanza atakayoanza nayo kwa sasa ni kushughulika na safu ya ushambuliaji ili irejeshe makali yake. Baraza amechukua mikoba ya Mecky Maxime ambaye alifutwa kazi kutokana na mwendo mbovu wa timu yake na mchezo wa mwisho kukaa benchi ilikuwa mbele ya Azam FC ambapo ubao wa Kaitaba ulisoma Kagera Sugar 1-2 Azam FC. Kwa sasa Maxime yupo huru ambapo amekuwa akitajwa kuibukia Biashara United kuchukua mikoba ya Baraza. Akizungumza na Saleh Jembe, Baraza amesema kuwa amewatazama washambuliaji wake walivyo na ameona ni lazima aanze nao ili kuongeza kasi kwenye ushambuliaji. "Ili timu ipate ushindi ni lazima ifunge na ufungaji unaanzia kwa washambuliaji pamoja na viungo ambao kazi yao ni kutengeneza nafasi za kufunga kwa washambuliaji. "Kikubwa ambacho nina amini kwamba kinawezekana ni kupata matokeo katika mechi zetu hivyo mashabiki watupe sapoti bila kuwa na mashaka nasi," . Kagera Sugar kwenye msimamo ipo...
Comments
Post a Comment